Gefundene Einträge
Buch | Kapitel | Vers | Text |
Matthaeus | 4 | 11 | Basi, Ibilisi akamwacha, na malaika wakaja, wakamhudumia. |
Matthaeus | 4 | 12 | Yesu aliposikia kwamba Yohane ametiwa gerezani alikwenda Galilaya. |
Matthaeus | 4 | 13 | Aliondoka Nazareti, akaenda Kafarnaumu, mji ulio kando ya bahari ya Genesareti, mpakani mwa wilaya za Zabuloni na Naftali, akakaa huko. |
Matthaeus | 4 | 14 | Ndivyo lilivyotimia lile neno lililosemwa kwa njia ya nabii Isaya: |
Matthaeus | 4 | 15 | "Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kuelekea baharini ng'ambo ya mto Yordani, Galilaya nchi ya watu wa Mataifa! |
Matthaeus | 4 | 16 | Watu waliokaa gizani wameona mwanga mkubwa. Nao walioishi katika nchi ya giza na kivuli cha kifo, mwanga umewaangazia!" |
Matthaeus | 4 | 17 | Tangu wakati huo Yesu alianza kuhubiri akisema, "Tubuni, maana ufalme wa mbinguni umekaribia!" |
Matthaeus | 4 | 18 | Yesu alipokuwa anatembea kando ya ziwa Galilaya, aliwaona ndugu wawili wavuvi; Simoni (aitwae Petro) na Andrea, ndugu yake; walikuwa wakivua samaki kwa nyavu ziwani. |
Matthaeus | 4 | 19 | Basi, akawaambia, "Nifuateni, nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu." |
Matthaeus | 4 | 20 | Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata. |
Matthaeus | 4 | 21 | Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona ndugu wengine wawili: Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Hao walikuwa ndani ya mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakitengeneza nyavu zao. Basi Yesu akawaita, |
Matthaeus | 4 | 22 | nao mara wakaiacha mashua pamoja na baba yao, wakamfuata. |
Matthaeus | 4 | 23 | Yesu alikuwa anakwenda kila mahali wilayani Galilaya, akifundisha katika masunagogi na kuhubiri Habari Njema juu ya ufalme wa Mungu. Aliponya kila namna ya maradhi na magonjwa waliyokuwa nayo watu. |
Matthaeus | 4 | 24 | Habari zake zikaenea katika mkoa wote wa Siria. Wagonjwa wote wenye maradhi ya kila namna na wale waliosumbuliwa na kila namna ya taabu: waliopagawa na pepo, wenye kifafa na watu waliokuwa wamelemaa, walipelekwa kwake; naye akawaponya wote. |
Matthaeus | 4 | 25 | Makundi mengi ya watu kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Yudea na ng'ambo ya mto Yordani, walimfuata. |