menu.png
Passwort vergessen ?

Bibel durchsuchen

 (Index)


Gefundene Einträge

•••► •••►
Buch Kapitel Vers Text
Matthaeus 4 11 Basi, Ibilisi akamwacha, na malaika wakaja, wakamhudumia.
Matthaeus 4 12 Yesu aliposikia kwamba Yohane ametiwa gerezani alikwenda Galilaya.
Matthaeus 4 13 Aliondoka Nazareti, akaenda Kafarnaumu, mji ulio kando ya bahari ya Genesareti, mpakani mwa wilaya za Zabuloni na Naftali, akakaa huko.
Matthaeus 4 14 Ndivyo lilivyotimia lile neno lililosemwa kwa njia ya nabii Isaya:
Matthaeus 4 15 "Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kuelekea baharini ng'ambo ya mto Yordani, Galilaya nchi ya watu wa Mataifa!
Matthaeus 4 16 Watu waliokaa gizani wameona mwanga mkubwa. Nao walioishi katika nchi ya giza na kivuli cha kifo, mwanga umewaangazia!"
Matthaeus 4 17 Tangu wakati huo Yesu alianza kuhubiri akisema, "Tubuni, maana ufalme wa mbinguni umekaribia!"
Matthaeus 4 18 Yesu alipokuwa anatembea kando ya ziwa Galilaya, aliwaona ndugu wawili wavuvi; Simoni (aitwae Petro) na Andrea, ndugu yake; walikuwa wakivua samaki kwa nyavu ziwani.
Matthaeus 4 19 Basi, akawaambia, "Nifuateni, nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu."
Matthaeus 4 20 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
Matthaeus 4 21 Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona ndugu wengine wawili: Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Hao walikuwa ndani ya mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakitengeneza nyavu zao. Basi Yesu akawaita,
Matthaeus 4 22 nao mara wakaiacha mashua pamoja na baba yao, wakamfuata.
Matthaeus 4 23 Yesu alikuwa anakwenda kila mahali wilayani Galilaya, akifundisha katika masunagogi na kuhubiri Habari Njema juu ya ufalme wa Mungu. Aliponya kila namna ya maradhi na magonjwa waliyokuwa nayo watu.
Matthaeus 4 24 Habari zake zikaenea katika mkoa wote wa Siria. Wagonjwa wote wenye maradhi ya kila namna na wale waliosumbuliwa na kila namna ya taabu: waliopagawa na pepo, wenye kifafa na watu waliokuwa wamelemaa, walipelekwa kwake; naye akawaponya wote.
Matthaeus 4 25 Makundi mengi ya watu kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Yudea na ng'ambo ya mto Yordani, walimfuata.

Seite:   1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11